KIGALI-RWANDA’
Na
Anatoli Salawa
Wito
umetolewa kwa waandishi wa habari na wataalamu wa tasnia ya habari wa Kanisa
Katoliki kutumia fursa za Teknolojia ya Habari na Mawasiliano kujenga utamaduni
unaoleta amani katika familia ya binadamu, kwa kuandaa maudhui yanayokuza
umoja, mshikamano na kuheshimu utu.
Hayo
yameelezwa na Askofu Mkuu wa JImbo Kuu la Kigali nchini Rwanda, Mwadhama ANTONI Kardinali KAMBANDA,
wakati wa uzinduzi wa Kongamano la Kimataifa la SIGNIS linaloendelea huko
Kigali nchini Rwanda.
Akitoa ujumbe wake katika Kongamano hilo, Kardinali Kambanda ameonya juu ya matumizi
mabaya ya vyombo
vya habari na kwa namna ya pekee kwa wakati huu ambapo mawasiliano ya
kidijitali yamekuwa ndiyo
nyenzo ya kufikisha ujumbe kwa muda mfupi kuliko wakati wowote.
Amesema
kuwa katika ulimwengu huu wa kidijitali vyombo vya Habari vinaweza kuwa nyenzo
zenye nguvu
na uwezo wa kubomoa na kuingiza hofu kwa jamii ya binadamu kwa haraka kama
vitasimamiwa na
watu wasio na nia njema ya kujenga na kuileta jamii pamoja na badala yake wakajikita katika kuboa misingi ya umoja, amani na mshikamano.
Ametolea mfano mauaji ya kutisha yaliyofanyika nchini Rwanda mnamo Mwaka 1994,kuwa yalichangiwa na chombo cha Habari ambacho kilichochea taharuki na mauaji ya kutisha ambayo yalileta machozi na maumivu kwa wanarwanda kwa miaka mingi.
Amewaasa wanahabari wa Kanisa Katoliki kubeba wajibu mkubwa wa kuendelea kuponya majeraha hayo kwa kuandaa maudhui ya upatanisho.
Aidha
ametoa wito kwa, waandishi wa Habari na wanaosimamia vyombo vya Habari vya
kanisa kuleta mabadiliko
katika tasnia ya Habari wakilenga kumkomboa mwanadamu mzima kimwili na Kiroho.
SIGNIS
Ni Shirika la Kanisa Katoliki linalosimamia Vyombo vya Habari na Wanahabari
katika Kanisa Katoliki
Ulimwenguni.
Zaidi ya wanahabari wa Kanisa katoliki miambili sitini kutoka
nchi mbalimbali duniani
wanashiriki Kongamano hilo, ambapo washiriki Zaidi ya ishirini ni wanahabari
Wakatoliki kutoka Tanzania.

Baadhi ya Maaskofu wakiwa kwenye Misa ya ufunguzi wa Kongamano

Wanahabari kutoka mataifa mbalimbali wakiwa kwenye Misa ya ufunguzi wa Kongamano

Mapadre ambao wengi wao ni wataalam wa masuala ya Habari na Mawasiliono kutoka mataifa mbalimbali wakiwa kwenye Misa ya ufunguzi wa Kongamano
Wanakwaya
Tanzania.
Post a Comment