POLISI SHINYANGA KUCHUNGUZA MADAI YA MAFUTA KUCHANGANYWA NA MAJI
Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga, kwa kushirikiana na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), linaendelea kuchunguza madai ya kuwepo kwa mafuta yaliyochanganywa na maji katika kituo kimoja cha mafuta mjini Shinyanga.
Kamanda wa
Polisi Mkoa wa Shinyanga, SACP Janeth Magomi, amesema uchunguzi huo unafanyika
kufuatia malalamiko ya wamiliki wanne wa magari waliodai magari yao kupoteza
nguvu baada ya kujaza mafuta katika kituo hicho.
Amesema
walalamikaji wanahisi mafuta waliyonunua huenda yalichanganywa na maji, hivyo
uchunguzi wa pamoja na wataalamu wa EWURA unaendelea ili kubaini ukweli wa
suala hilo.
Kamanda
Magomi amewataka wananchi kuwa watulivu wakati uchunguzi ukiendelea,
akisisitiza kuwa majibu sahihi ya kisayansi yatatolewa baada ya kukamilika kwa
uchunguzi wa kitaalamu.

Post a Comment